Leo Lazima Yanga Tuwaangamize Mapema - Kapombe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Leo Lazima Yanga Tuwaangamize Mapema - Kapombe
BEKI wa Simba, Shomary Kapombe, amesema kwa sasa anaendelea vizuri na majeraha ya nyonga yaliyokuwa yakimsumbua baada ya kupona na yupo tayari kuanza mapambano na kwamba leo Simba itashinda tu kwani wachezaji wenzake waliopo wana uwezo mkubwa.

Kapombe ambaye mara kwa mara amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo, hivi karibuni alijitonesha wakati akiitumikia timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ilipocheza dhidi ya Rwanda kwenye mchezo wa kusaka tiketi ya kushiriki Michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (Chan).
Akizungumza na Championi Jumatano, Kapombe amesema mchezo wa leo mbele ya watani zao, Yanga ana imani kubwa na kikosi kilichopo hivyo ana matarajio makubwa na ushindi.

“Kwa sasa naendelea vizuri kwani yale majeraha yangu yamepona na sisikii maumivu, muda wowote naweza kuungana na wenzangu kwa ajili ya mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao, sifurahii kukaa nje, nimekuwa nikipambana kuhakikisha napona haraka na kurejea uwanjani kuipambania timu yangu, kitu cha faraja ni kwamba kwa sasa naweza kufanya hivyo kutokana na kupona.
“Kuhusu mchezo wa leo wa Ngao ya Jamii nina imani na wachezaji wenzangu watatuwakilisha kwa ushindi hivyo, sina hofu kwani timu yangu ina uwezo wa kushinda bila mimi,” alisema Kapombe.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad