Mauno ya Moses Iyobo Yampagawisha Aunty Ezekiel Mpaka Kuikana Ndoa Yake Sunday Demonte

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mapenzi ya Iyobo Yapelekea Aunty Ezekiel Kuikana Ndoa Yake
Siku chache baada ya kuenea kwa madai kuwa mume wa ndoa wa mkali wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel, Sunday Demonte ameachiwa huru huko Dubai baada ya kutumikia kifungo cha miaka kadhaa huku staa huyo akishi kinyumba na mwanaume mwingine, muigizaji huyo amesema ndoa hiyo haipo tena.

Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Aunt ambaye alifunga ndoa na Demonte yapata miaka minne iliyopita, alisema kuwa, anawashangaa watu wanaoikomalia ishu hiyo ambayo kwa upande wake ni ndogo.

Ngoja niulize, hivi jamani mbona watu siyo waelewa? Nani asiyejua kama mimi niko na mtu hivi sasa?

Na ninaamini kabisa hata yeye (Demonte) anajua? Kwa hiyo hata kama ameachiwa huru na akaja, ukweli utabaki kuwa ndiyo huohuo tu, kwamba tayari nina mtu mwingine maana hata yeye asingeweza kusubiri muda wote huo, hivyo ajue tu hana chake,” alisema Aunt.

Staa huyo aliongeza kuwa, kwa hivi sasa ni vigumu kuachana na mzazi mwenziye aliyenaye kwa kuwa tayari wana mtoto ambaye anapenda kuwaona wakiwa pamoja, hivyo hawezi kumtesa mwanaye.

Hebu fikiria, mtoto wangu amezoea kutuona pamoja mimi na baba yake na ni kitu ambacho anakipenda sana, sasa kwa nini nimuumize?” alihoji Aunt.

Risasi Mchanganyiko baada ya kuzungumza na Aunt, lilimtafuta mzazi mwenziye huyo ili azungumzie ujio wa mume wa ndoa wa mpenzi wake, lakini alisema yeye hana cha kuzungumza, isipokuwa mwenye uamuzi wowote ni Aunt.

Unajua kwenye jambo kama hilo mtu anayeweza kuzungumza vizuri ni Aunt mwenyewe na yeye ndiye mwenye uamuzi wote, ninachojua mimi ni baba mtoto na itabaki kuwa hivyo siku zote,” alisema kijana huyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad