Mfanyabiashara Kizimbani kwa Kukutwa na Sare za JWTZ

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA






Mfanyabiashara Kizimbani kwa Kukutwa na Sare za JWTZ
Casto Onyomolile Ngogo (35) mfanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es salaam, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shtaka la kukutwa na suruali 5,000 za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).



Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kwa Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba alidai kuwa Ngogo ambaye ni mkazi wa Tabata Segerea,  alikutwa na vifaa hivyo katika maeneo ya bandari kavu ya Galco Inland Container (ICD) iliyopo Sokota Chang’ombe Juni 15 mwaka huu .

Wakili wa Serikali, Simon alidai kuwa siku hiyo, mshtakiwa huyo alikutwa na suruali 5,000 za JWTZ zenye thamani ya Shilingi 50 milioni ambazo zimepatikana kwa njia isiyo halali.

Juni 15 mwaka huu, Ngogo anadaiwa kuwa katika eneo hilo alikutwa na maofisa wa Jeshi la Polisi akiwa na tisheti 50 za JWTZ zenye thamani ya Shilingi 500, 000.

Hata hivyo mshtakiwa  hakuruhusiwa kusema chochote kwa sababu shtaka lake Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad