Mkwasa Atoa Neno Kuhusu Kupigwa Mnada Jengo la Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mkwasa Atoa Neno Kuhusu Kupigwa Mnada Jengo la Yanga
Katibu Mkuu wa Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga, Charles Boniface Mkwasa amekiri kuwa klabu yao inadaiwa kodi na serikali huku akiwataka mashabiki na wanachama wa jangwani kuwa watulivu katika kipindi hiki.

Mkwasa amebainisha hayo leo baada ya taarifa kuwepo taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu jengo lao kupigwa mnada siku ya Jumamosi
“Ni kweli tuna deni kubwa tunadaiwa na ardhi lakini tayari tulifanya nao mazungumzo na kukubaliana namna ya kulilipa kupitia mapato yetu ya milangoni. Tatizo ni kwamba hapa katikati ligi ilisimama, lakini hivi karibuni inaanza na tutaendelea kulipa, Tutatoa taarifa rasmi baadaye”, alisema Mkwasa.

Mkwasa amesema kiasi wanachodaiwa ni kikubwa lakini hakizidi shilingi milioni 500, huku akiweka wazi kuwa pesa wanayotakiwa kulipa kwa mwaka ni shilingi milioni 59.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia kwa kampuni ya udalali ya Msolopa Investmenst Limited leo imetangaza kulipiga mnada jengo hilo endapo Yanga hawatalipa kabla ya Agosti 19, mwaka huu.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad