Msemaji wa Jeshi Aliyedaiwa Kutoweka Ajitokeza Kenya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wizara ya ulinzi nchini Kenya imeshutumu taarifa zilizokuwa zimeenezwa kwamba msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Joseph Owuoth alikuwa ametoweka.

Waziri Raychelle Omamo, akihutubia wanahabari, amesema taarifa kama hizo zinatishia usalama na kuzua wasiwasi miongoni mwa maafisa wa jeshi na familia zao.

"Kanali J. M. Owuoth hajatoweka na yuko nasi hapa, akiwa hai na mzima wa afya," alisema Bi Omamo.

Kanali Owuoth aligonga vichwa vya habari baada ya kuthibitisha kwamba nyaraka zilizokuwa zimetumiwa na muungano wa upinzani nchini humo Nasa kudai kwamba serikali inapanga kutumia jeshi kutekeleza 'mapinduzi' ili kuendelea kusalia madarakani zilikuwa halisi.

Msemaji huyo hata hivyo alisema nyaraka hizo zilinukuliwa na kufasiriwa visivyo.
Bi Omamo, kwenye kikao hicho, alisema baada ya uchunguzi, imebainika kwamba nyaraka hizo zilizotumiwa na muungano wa Nasa zilikuwa ghushi.

Taarifa za kudaiwa kutoweka kwa Kanali Owuoth zilikuwa zimezua wasiwasi mkubwa kwani zilijiri siku moja baada ya mwili wa meneja wa teknolojia katika Tume ya Uchaguzi Kenya (IEBC) Chris Msando, aliyetoweka Ijumaa usiku, kupatikana katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City jijini Nairobi pamoja na mwili wa mwanamke mwingine.

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati aliambia wanahabari kwamba hakukuwa na shaka kwamba Bw Msando aliteswa kabla ya kuuawa na kuwataka polisi wafanye uchunguzi wa kina kufumbua kitendawili kuhusu kuuawa kwake.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad