Mzungu Akosa Dhamana Aendelea Kusota Rumande

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mzungu Akosa Dhamana Aendelea Kusota Rumande
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, le0 Agosti 18, 2017 imemnyima dhamana raia wa Afrika Kusini ambaye ni mhandisi, Menelaos Tsampos, anayetuhumiwa kwa kosa la kumtishia mtu kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa kompyuta.

Upande wa utetezi unaoongozwa na wakili Deus Singa ulikuwa ukiiomba mahakama hiyo kumpa dhamana Menelaos wakati kesi yake ikiendelea, huku upande wa mashitaka ukipinga kupewa dhamana kwa kile walichokieleza kuwa akiachiwa huru anaweza kumdhuru aliyemtishia maisha.
Kutokana na hoja hizo, hakimu aliiahirisha kesi hiyo hadi kesho Agosti 18, 2017 ambapo itaelezwa iwapo atapewa dhamana. Mshitakiwa wamerudishwa rumande.

Menelaos anadaiwa mahakamani hapo kuwa Juni 22, mwaka huu maeneo ya jijini Dar es Salaam, kupitia mfumo wa kompyuta alituma ujumbe wa baruapepe (E-mail) uliokuwa na maneno ya vitisho kwa mtu anayeitwa Costa Gianna, ikiwa ni kinyume na sheria ya mtandao kifungu cha 23(1) na (2) namba 14 ya mwaka 2015.

Mzungu huyo amekua gumzo mahakamani hapo alipoanzisha timbwili kortini hapo juzi baada ya kuwachimba mkwara mzito waandishi wa habari waliokuwa wakimpiga picha siku ya kwanza alipofikishwa mahakamani0.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad