AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msuva amesema kwamba katika mchezo huo uliofanyika wa El Abdi mjini Jadida, yeye amefunga bao moja ambalo lilikuwa la kusawazisha na kuseti la ushindi.
“Tumeshinda mabao 2-1, maana huku kila siku tunacheza mechi, kweli wenzetu wapo tofauti sana,”amesema Msuva na kuongeza; “Leo mimi nimefunga la kusawazisha na kutengeneza la ushindi,”.
Msuva amesema mechi zote wanazocheza za kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Morocco, maarufu kama Botola dhidi ya timu tofauti, zikiwemo za Daraja la Kwanza ni ngumu.
“Ni mechi ngumu, timu za huku wachezaji wake wapo fiti sana na wana nguvu na kasi sana, kwa kweli huku wenzetu wapo tofauti sana,”alisema.
Awali ya hapo, Msuva alishiriki zoezi la kutambulisha jezi mpya za Jadida za msimu ujao pamoja na wachezaji wenzake wengine watatu walioteuliwa.
Zoezi jilo lilifanyika katika mkutano na Waandishi wa Habari mabao makuu ya klabu. Ikumbukwe ni wiki iliyopita tu Msuva amesaini mkataba wa miaka mitatu kujiunga na DHJ kutoka Yanga ya Tanzania.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK