CRDB Yampa PAUL Makonda Milioni 100 Kusaidia Ujenzi wa ofisi za Walimu kwa Shule za Msingi na Sekondari

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

CRDB Yampa PAUL Makonda Milioni 100 Kusaidia Ujenzi wa ofisi za Walimu kwa Shule za Msingi na Sekondari
Paul Makonda
Benki ya CRDB leo Jumatatu imekabidhi msaada wa Sh100 milioni kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa ofisi za walimu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa.

Mbali na kukabidhi fedha hizo, mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo, DK Charles Kimei ameahidi kuongeza Sh100 milioni katika bajeti ijayo.

"Mwalimu ndio chanzo cha maarifa ya kila mtu, tukitengeneza mazingira mazuri ya ufanyaji kazi kwake hata elimu inayotolewa itakua na kiwango," amesema Dk Kimei.

Amesema ili Taifa liweze kusonga mbele kimaendeleo ni lazima kuwekeza katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu na kuweka mazingira bora ya ufundishaji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi ya Mkoa wa Dar es Salaam, Kanali Charles Mbuge alimhakikishia Dk Kimei kuwa pesa zilizotolewa zitafanya kazi iliyokusudiwa.

"Thamani ya pesa iliyotolewa italingana na kile kitakachofanyika na hii iwe chachu kwa benki nyingine kuweza kuchangia ujenzi huu," amesema Kanali Mbuge.

Mkoa wa Dar es Salaam una jumla ya shule 638 zikiwa na upungufu wa ofisi 402 za walimu.

Chanzo: Mwananchi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Paul Makonda, au Bashite sijui ni nani kati ya hawa wawili ni mcha Mungu, msemakweli. Na simjui kati ya hawa wawili ni kinyonga. Kinachonishangaza, Kati ya Wakuu wa mikoa yote ya Tanzania, Ni Paul makonda tu anayepata misaada kutoka mashirika, makampuni na Wachina . Zidi ya mkuu wa mkoa yeyote. Kuna kitu kimejifificha nyuma ya huyu Bashite Paul kikubwa sana na kwa hali ya juu inabidi asifiwe kila siku wakifikiri Watanzania watasau ni nani huyu kijana, na nini amekifanya hadharani, na kinaphitaji kupakwa mafuta matakatifu juu ya uozo fulani. Kitanuka tu,. Msijidanganye.

    ReplyDelete

Top Post Ad