Kwa Hali Ilivyo Sasa Tanzania ni Wazi Amani Haipo Kama Zamani- Jay Dee

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kwa Hali Ilivyo Sasa Tanzania ni Wazi Amani Haipo Kama Zamani- Jay Dee
Msanii mkongwe wa muziki wa bongo fleva Lady Jaydee amefunguka na kusema kwa hali ilivyo sasa Tanzania ni wazi kuwa amani haipo kama alivyokuwa kipindi cha nyuma na kudai hali hiyo inaleta hofu miongoni mwa wananchi.

Lady Jaydee alisema hayo kwenye kipindi cha Planet bongo na kusema kitendo cha Mbunge Tundu Lissu pamoja na Meja Jenerali mstaafu wa JWTZ, Vincent Mritaba kupigwa risasi na watu wasiojulikana ni wazi kuwa amani ya nchi haipo.

"Ni kweli Tanzania hakuna amani kwa sababu kitendo cha mtu kupigwa risasi hadharani inatishia amani ukizingatia kuna wasanii wengine walikuwa wanatekwa unaogopa, sehemu yenye amani vitu kama hivyo haviwezi kutokea, na kitendo cha Meja mstaafu wa JWTZ kupigwa naye risasi inaongeza kabisaa Tanzani kuwa amani haipo naweza kuwa sina la kusema ila nikaishia kusikitika tu" alisema Lady Jaydee
Aidha Lady Jaydee anasema matukio haya yanaotoa picha mbaya kuwa kama nchi tunakokwenda si sehemu nzuri
Mbali na hilo Lady Jaydee kwa sasa ameachia video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la 'I miss you' uliotengenezwa na mtayarishaji Man Water kutoka Combination Soound.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad