Lema' Nassari ni Wabunge Halali Tushikamane Kuleta Maendeleo- JPM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Lema' Nassari ni Wabunge Halali Tushikamane Kuleta Maendeleo- JPM
Rais Magufuli amewazungumzia wabunge wawili wa (CHADEMA) Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema pamoja na Mbunge  wa jimbo la Arumeru Mashariki Mhe. Joshua Nassari kuwa ni wabunge halali wa majimbo hayo kwa kuwa wananchi ndiyo waliwachagua.

Rais Magufuli amesema hayo leo aliposimamishwa na wananchi wa Sangisi katika kata ya Akeri nje kidogo ya Mji wa Arusha akiwa njiani kurejea jijini Dar es Salaam leo Asubuhi na kusema yeye atabaki kuwa Rais wala hawezi kubadilika na kuendelea kuwatumikia Watanzania wote.
"Uchaguzi umeshakwisha sasa ni maendeleo mliamua mkamchagua Magufuli na ndiyo Rais na mimi nitakuwa Rais wala sibadiliki na nitawatumikia Watanzania wote, mliamua mkamchagua Mhe. Lema wa CHADEMA kuwa Mbunge wenu yule ni Mbunge halali, mkaamua kumchagua Nassari kuwa Mbunge wenu ni Mbunge halali kwa hiyo tushikamane sisi kama Watanzania kuleta maendeleo yetu uchaguzi ulikwisha tusubiri mwaka 2020" alisema Rais Magufuli
Mbali na hilo Magufuli amewataka Watanzania kuleta maendeleo ya kweli bila kubagua vyama na kubagua dini zetu na bila kubagua makabila na kusema yeye kama kiongozi wa nchi hajaweza kuwabagua na ndiyo maana anafanya mambo ya maendeleo katika majimbo hayo ikiwa ni pamoja na kupeleka barabara

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Watu wanauelewa sana mchango wa viongozi hawa. Inasikitisha watu waogope kuwathamini lakini si kweli. Michango yao ni mikubwa sana huku bado wakijiendeleza kimasomo. Wana kiu kubwa ya kuwapatia watu wao maendeleo yanayoenda na wakati. Ni wadhamiria ambapo ungewaunga mkono toka mwanzo ukafanya nao pamoja kama Watanzania, bila kujali rangi za chama, utafaidika sana sababu utawategemea wao kufanya kazi na wananchi wao.Itakupunguzia mzigo mkubwa sana.

    ReplyDelete

Top Post Ad