AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kiongozi wa muungano huo Raila Odinga ametangaza kuwa, hawatakubali kufanyika kwa Uchaguzi huo iwapo Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Ezra Chiloba na maafisa wengine wataendelea kuandaa uchaguzi mpya.
Naibu rais William Ruto ambaye pia ni naibu kiongozi wa chama cha Jubilee ameshutumu kauli ya Odinga na kueleza ni mbinu ya kiongozi huyo wa upinzani kutotaka Uchaguzi.
Mvutano wa kisiasa unaendelea nchini Kenya, huku ikiripotiwa kuwa Tume ya Uchaguzi inapanga kukutanana wawakilishi wa pande zote mbili za kisiasa, kukubaliana kuhusu maandalizi ya Uchaguzi mpya.
Wakati uo huo, kiongozi wa mashtaka nchini Kenya Keriako Tobiko, ameagiza kuchunguzwa kwa Tume ya Uchaguzi nchini Kenya baada ya kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi wa urais mwezi uliopita.
Tobiko ameagiza Polisi na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi kuchunguza iwapo wafanyikazi wa Tume hiyo waliohusika na udanganyifu uliosababisha matokeo hayo kufutwa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Hivi hawa watu watafanya kazi kweli? Mara maandamano-mara marudio uchaguzi......duh litawachwea....tahamaki 2020 hii, tunafanya nao pamoja uchaguzi.....
ReplyDelete