AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Edward Chegero amesema leo Alhamisi kuwa, wahamiaji hao walikamatwa Kongowe wilayani Temeke.
Amesema wamekamatwa jana Jumatano baada ya idara kupata taarifa na baadaye kuweka mtego uliowanasa.
Chegero amesema mbali na wahamiaji hao, idara imewakamata Watanzania wanne waliokuwa wakiwasindikiza wahamiaji hao.
Amesema Watanzania hao walikuwa wakitumia gari aina ya Toyota Passo.
Kaimu kamishna amesema uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wahusika wote wa mtandao huo.
Chegero amesema baadhi ya wahamiaji hao walikuwa na tiketi zinazoonyesha wanatoka Msata kwenda Dar es Salaam.
Amewataka madereva wa malori na usafiri mwingine kutosafirisha wahamiaji haramu kwa kuwa kufanya hivyo ni kuvunja cha sheria.
Kaimu kamishna pia amewaonya wamiliki wa nyumba za wageni zinazotumika kuwaficha wahamiaji hao akisema kiama kwao kinakuja.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK