Mashabiki Waitupia Lawama TFF Mechi ya Simba na Azam FC Kupelekwa Azam Complex

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mashabiki Kuitupia Lawama TFF Mechi ya Simba na Azam FC Kupelekwa Azam Complex
Mashabiki wa soka wamelalamika kitendo cha mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Simba dhidi ya Azam FC kupelekwa Azam Complex, Chamazi.

TFF imeamua kutangaza michezo ya Simba na Yanga dhidi ya Azam FC, sasa nayo itakuwa inachezwa Azam Complex tofauti na awali kutokana na ukubwa wake ilitakiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Taifa au ule wa Uhuru.

Safari hii, Azam FC itaikaribisha Simba Chamazi katika mechi itakayopigwa Jumamosi ikiwa ni ya pili ya Ligi Kuu Bara msimu huu kwa kila timu.

Mashabiki hao walioandika maoni katika mitandao ya Kijamii ya Salehjembe pamoja na blog yenye ya Salehjembe wamelia kutotendewa haki.

Kwa ujumla mashabiki hao wamelalamika kuhusiana na udogo wa uwanja wa Azam Complex wenye uwezo wa kuchukua watu 7,000.

“Nafikiri hii si sawa, wote tunajua uwanja huo ni mdogo na hii ni mechi kubwa. Wanatunyima haki ya kuona mechi hiyo.

“Angalau kungekuwa hakuna viwanja, lakini kuna Uhuru upo pale.”

Wengine walilalamikia umbali wa Chamazi na muda ambao mechi imepangwa Saa 1 usiku.

Lakini Azam FC imekuwa na kilio cha kutaka kucheza mechi zake nyumbani jambo ambalo hatimaye limetimia.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad