AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Habari kutoka kwenye chanzo cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa staa huyo zilieleza kuwa, dili hilo alilopata Wema ni kwa ajili ya kutengeneza tamthilia na sinema kupitia kampuni yake ya Endless Fame ambazo zitaruka kwenye kituo hicho na kuambulia donge hilo nono.
“Wema sasa hivi atakuwa mtu mwingine kabisa kwa sababu dili hilo akikabidhiwa kabisa atarejea kwenye ile status yake ya kuitwa pedeshee mwanamke na hata marafiki waliokuwa wameyeyuka watarudi,” kilinyetisha chanzo hicho.
Mpashaji huyo aliendelea kufunguka kuwa, Wema anatarajia kuwakusanya kampani yake yote ya Endless Fame kwa ajili ya tenda hiyo ambayo itakuwa ni ya aina yake.
Baada ya kudaka habari hizo njema kuhusu Wema ambaye wengine humuita ‘Keki ya Taifa’ au ‘Tanzania Sweetheart’, Ijumaa Wikienda lilimsaka lakini halikufanikiwa badala yake lilimpata mmoja wa waratibu wa kazi zake ambaye alikiri kuwepo kwa dili hilo, lakini bado halijakamilika mpaka leo (Jumatatu).
“Duh! Ninyi noma, mmeinyaka? Ni kweli hilo dili lipo, lakini nafikiri litakamilika Jumatatu ijayo (leo),” alinyetisha mdau huyo.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, simu ya Wema ilikuwa ikiita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa SMS hakuwa amejibu
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mungu wetu sote, na humpa amtakae, hata ukimzibia leo kesho atanyookewa. Wema kwa uzuri na roho yako ya kusaidia watu hutokufa maskini. Limmemshuka Bashite alifikiri yeye Mungu mtu. malipo duniani.
ReplyDeletemmhh km ni kweli all the best tz sweetheart''
ReplyDelete