Serikali Yatoa Msaada wa Nyumba kwa Askari Polisi Waliounguliwa Moto

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Yatoa Msaada wa Nyumba kwa Askari Polisi Waliounguliwa Moto
Serikali kupitia wakala wake wa ujenzi nchini (TBA) imetoa msaada wa nyumba kwa askari polisi waliounguliwa nyumba zao hapo jana, mpaka pale watakapopata makazi rasmi.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa East Africa Radio, na kusema baada ya ajali hiyo askari hao walikosa mahali pakuishi, hivyo wanaishukuru TBA kwa msaada huo.
"Ule moto umeteketeza kila kitu kabisa, hivyo wale askari hawakuwa na sehemu ya kuishi, jana tuliwahifadhi kwenye bwalo letu la polisi, lakini leo wamepatiwa msaada na wakala wa ujenzi wa serikali (TBA ), wamepewa nyumba za kuishi kwa muda hadi pale watakapopatiwa makazi rasmi, tunashukuru kwa hilo", amesema Kamanda Mkumbo.
Tukio la kuteketea kwa nyumba hizo limetokea usiku wa Septemba 27 mwaka huu  majira ya saa mbili na kuteketeza nyumba hizo, lakini jeshi la zimamoto liliwahi eneo la tukio na kutoa msaada kwa wananchi ambao walianza kuzima.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad