Upinzani Kenya Waitisha Maandamano Makubwa Wiki Ijayo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Upinzani Kenya Waitisha Maandamano Makubwa Wiki Ijayo
Muungano wa upinzani nchini Kenya umeitisha maandamano ya umma kupinga mapendekezo ya kuifanyia mabadiliko sheria ya uchaguzi.

Wabunge wanaoegemea upande wa serikali wanafanya hima kupitisha mswada ambao utamwezesha Uhuru Kenyatta kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa upinzani utasusia marudio ya uchaguzi tarehe 26 mwezi Oktoba.

Wanachama wa upinzani walitoka nje wakati upande wa serikali ukitumia wingi wake bungeni kuharakisha mabadiko ambayo yatasababisha mswada huo kuwa sheria kabla ya marudio ya uchaguzi.

Kati ya yale yaliyo kwenye mswada huo ni kuruhusu mgombea kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa mgombea mwingine atasusia uchaguzi.

Viongozi wa upinzani Kenya wazuiwa kwenye uwanja wa ndege Nairobi
Upinzani kuandamana Kenya
''Zaidi ya 100 walifariki'' katika maandamano Ethiopia
Marudio hayo ya uchaguzi yana wagombea wawili, Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.
Mswada huo pia unasema kuwa mahakama ya juu haiwezi kufuta matokeo ikiwa mfumo wa eletroniki utafeli
Kufeli kwa mfumo wa kupiga kura kwa njia ya eletroniki ndio ilikuwa sababu kuu ya kufutwa kwa matokeo ya urais.

Mgombea wa Upinzani Raia Odinga amekashifu hatua hizo kama jaribio la kuiba kura na kumpendela rais Uhuru Kenyatta.
Ametisha maandamano ya kote nchini kila Jumatatu na Ijumaa kuanzia wiki ijayo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad