AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Amesema hayo alipofunga mkutano wa 37 wa ngazi ya mawaziri wa nishati na madini wa nchi wanachama wa Kituo cha Madini Afrika (AMGC) uliolenga kujadili mchango wa sekta ya madini katika maendeleo ya bara hilo.
Mkutano huo umefanyika leo Alhamisi katika kituo cha AMGC kilichopo jijini hapa, Tanzania ikiwa mwenyekiti.
Waziri mkuu amesema licha ya nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania kuwa na utajiri wa madini, sekta hiyo haina tija kwa maendeleo hivyo ameagiza kuandaliwa mikakati madhubuti.
"Bara la Afrika lina utajiri mkubwa wa madini, sehemu kubwa ya madini hayo hayajatumika. Tanzania ina madini mengi kama vile dhahabu, almasi na Tanzanite lakini mchango wake ni asilimia nne pekee," amesema.
Kutokana na hali hiyo, amezitaka nchi wanachama wa AMGC kuandaa mikakati ya pamoja ili madini yawanufaishe wananchi.
"Changamoto iliyopo ni jinsi gani tunaweza kusimamia sekta hizi na kuleta maendeleo kuliko kuacha mashimo na umasikini," amesema.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani amesema wamepokea maagizo hayo na kuanzia mwakani watatumia kituo hicho kuchenjua mchanga wa madini na kufanya uyeyushaji.
"Nitoe wito kwa kampuni za madini na wachimbaji wadogo kuanza kuleta madini kwenye kituo hiki kwa ajili ya kuongeza thamani na kufanya uchambuzi," amesema
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK