AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum jijini Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, ambapo pia amelaani vikali kitendo cha askari wa jeshi la polisi kuvamia wananchi na kuwapiga, akisema si jambo sahihi kwa askari kufanya hivyo na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
"Tunalaani vikali mauaji ya askari wa polisi wa FFU kikosi cha Ukonga, lakini sambamba na hilo jeshi la polisi linalaani vitendo vya kihuni vya wananchi kushambuliwa, kuna watu wahuni ambao wanasambaa usiku wanakamata wananchi, kuwapiga na kuwadhalilisha kina mama na wengine kujeruhiwa, hakuna askari wa jeshi la polisi aliyefundishwa anayeweza kuyafanya hayo yanayoelezwa kufanyika, na kama atabainika ni kweli ni askari, watakamatwa, watahojiwa na tutawashughulikia kijeshi na kama wahalifu wengine watafikishwa mahakamani", amesema Kamanda Mambosasa.
Kamanda Mambosasa ameendelea kwa kusema kwamba jeshi hilo linaendelea na upelezi dhidi ya watu waliomuwa askari wake Charles Yanga wa kikosi cha Ukonga, na watakapobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK