AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Ijumaa mapema wiki hii akiwa katika mazungumzo na warembo waliokuwa wakishiriki kinyang’anyiro cha kumsaka Miss Ubungo 2017 yaliyofanyika Ukumbi wa JBN, Kijitonyama jijini Dar, Diana ambaye kiasili ni Mmasai alisema kuwa, tukio hilo hatalisahau kwa kuwa alifanikiwa kuchoropoka mikononi mwa ndugu zake hao waliotaka kuhakikisha anafanyiwa tohara hiyo kama wenzake. “Kwa mila za kwetu mwanamke ukifikia umri fulani ni lazima afanyiwe ukeketaji.
Kwangu mimi sikutaka kabisa kitu kama hicho kinitokee lakini kitendo cha kutia mguu nyumbani kwetu hivi karibuni huko Sakina, ndugu pamoja na watu wengine walinifuata na kunitaka nikeketwe, kisa kutimiza mila.
“Hata hivyo, nilifanikiwa kutoka mikononi mwao japokuwa hadi sasa hivi bado kuna ndugu wanaendelea kushikilia msimamo wa mimi kufanyiwa hivyo, lakini mwisho wa yote sikukubali kufanyiwa mambo yaliyopitwa na wakati,” alisema Diana huku akilengwa na machozi. Diana alikuwa Miss Tanzania mwaka jana katika kinyang’anyiro kilichofanyika jijini Mwanza akiwakilisha Wilaya ya Kinondoni.
Stori: Richard Bukos
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK