Rais Magufuli Amehudhuria Misa Kanisa Katoriki Jimbo la Zanzibar Askofu Atoa Neno Juu ya Utendaji Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais Magufuli Amehudhuria Misa  Kanisa Katoriki Jimbo la Zanzibar Askofu Atoa Neno Juu ya Utendaji Wake
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar, Agustino Shao amewataka Watanzania kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa hatua anazochukua za kurekebisha mambo muhimu kwa maendeleo ya Taifa, licha ya kuwepo changamoto katika kipindi cha mpito.

Ametoa ushauri huo leo Jumapili akihubiri wakati wa misa iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, Parokia ya Minaramiwili ambayo imehudhuriwa na Rais Magufuli.

Askofu Shao amesema hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli za kupambana na rushwa, kupigania rasilimali za Watanzania, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji, kukabiliana na wizi na ubadhilifu wa mali za umma na kubana matumizi zinapaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.

“Hatutaweza kusema tunaimaliza rushwa wakati tunaendelea kuishi kwa kupata fedha ambazo hujazifanyia kazi, ni lazima tuishi machungu ya kuimaliza rushwa, ni lazima tuishi machungu ya kuweka uadilifu katika utendaji wetu, tusipoishi machungu hayo tutaishi dunia mbili, dunia ya rushwa na dunia ya kujenga uchumi na uadilifu wa Watanzania,” amesema.

Taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari imesema baada ya misa kumalizika Rais Magufuli amemshukuru Askofu Shao kwa mahubiri.

Amewahakikishia Watanzania kuwa Serikali inachukua hatua za kupambana na rushwa na kulinda rasilimali za nchi ili ziweze kuwanufaisha wananchi.

Rais Magufuli amesema Baba wa Taifa, Julius Nyerere ambaye jana Jumamosi iliadhimishwa miaka 18 tangu kifo chake alipiga vita rushwa na alipigania rasilimali za nchi, hivyo ametaka Watanzania wote kuungana katika juhudi hizo.

Dk Magufuli amechangia Sh1 milioni kwa ajili ya kwaya ya kanisa hilo na Sh5 milioni  kwa ajili ya maendeleo ya kanisa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad