AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rage mapema wiki hii, aliliambia gazeti hili kwamba, Mkude ana kiwango kikubwa hivyo anapaswa kuchezea moja kati ya timu kubwa za Afrika hata TP Mazembe ya DR Congo au Raja Casablanca.
Alisema Mkude ni mmoja wa wachezaji wenye uwezo Simba ambaye amekuwa akimtabiria kufika mbali zaidi iwapo atajituma zaidi ili kuweza kucheza nje.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Mkude alisema kauli hiyo ya Rage imemzindua na sasa anapambana kufa na kupona aweze kupata nafasi ya kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.
“Rage alikuwa mwenyekiti wangu kwa muda wa miaka minne, hivyo ananifahamu vizuri kiwango changu, tena zaidi ya sana, tangu alipokuwa akiongoza.
“Amenipa hamasa kubwa ya kuweza kujituma na kupambana niweze kufanya vizuri kwa ajili yangu, familia yangu na kwake pia, nimeupokea ushauri wake kwa mikono miwili na ninashukuru kwa kunikumbusha.
“Ninajituma zaidi ikiwa ni sehemu ya kujiandaa kuondoka Simba kwenda nje ya nchi kucheza soka la kulipwa na naamini nitatimiza ndoto zangu hizi, naomba Mungu anisaidie,” alisema Mkude.
Mwanzoni mwa msimu huu, Mkude alisaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba baada ya ule wa awali kuisha.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mkude hayo maneno ya Rage wala yasimvimbishe kichwa. Kwa kuangalia kwa haraka Tanzania hakuna club yenye baraka kama Simba kwa nchezaji mwenye kujitakia maendeleo yakwenda kucheza nje ya Tanzania sema vijana au wachezaji wetu ni wazembe. Yeye Mkude mwenyewe ndie aliejicheleweshea maendeleo. Kama ameamka na kundua kuwa ameshachelewa basi asisubiri kujiremba na aanze safari kwa bahati Simba inashiriki mashindano ya kimataifa na aonyeshe uwezo wake huko kwani ndiko atakapoonekana na kina mazembe nakadhalika.
ReplyDelete