AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa kutoka kwenye gazeti la Tribune la nchini humo zinaeleza kuwa kaka wa msichana huyo aliyetembezwa akiwa uchi, alifanya mapenzi na binti wa familia nyingine hivyo baraza la kijiji liliamuru kaka huyo alipe kiasi cha rupia 150,000 za Pakistan sawa na Tsh milioni 2.2 mwaka jana ili kuyamaliza matatizo hayo kifamilia.
Hata hivyo familia ya Mwanaume huyo mzinifu aliyetambulika kwa jina la Sajjad ilishindwa kutoa fedha hizo ndipo baraza hilo la kijiji lijulikanalo kama (Panchayati) lilipotoa hukumu hiyo ya kumtembeza dada wa Sajjad uchi wa mnyama mbele ya wanakijiji ili liwe funzo kwa familia nyingine.
Tayari polisi nchini Pakistan wametangaza kuwakamata watu saba kufuatia tukio hilo la udhalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia, wengi wa waliokamatwa ni viongozi wa baraza la kijiji waliotoa hukumu hiyo.
Matukio kama hayo sio mageni nchini Pakistan hii kutokana na msimamo na maamuzi makali ya mabaraza ya vijiji nchini humo kuwakandamiza wanawake.
Mwaka 2002 kulitokea hukumu ya ajabu kama hiyo ambapo mwanamke mmoja ajulikanae kwa jina la Mukhtar Mai aliamriwa kubakwa na kundi la vijana ingawaje alienda kutoa taarifa mapema Polisi.
Mabaraza ya vijiji nchini humo yamekuwa yakitumika kusuluhisha kesi mbalimbali kwenye jamii huku yakilaumu kuwa mahakama nchini humo ni dhaifu katika utendaji ingawaje serikali nchini pakistani haitambui uwepo wa mabaraza hayo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Sio haki kabisa.kosa afanye mwengine aadhibiwe mwengine.ukosefu wa maadili.
ReplyDelete