Peter: Sihusiki na Kundi la P-Square Kuvunjika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

NYOTA wa muziki nchini Nigeria ambaye alikuwa anaunda kundi la P-Square, Peter Okoye, ameweka wazi kuwa yeye si chanzo cha kundi hilo kuvunjika.

Kundi hilo kwa sasa limevunjika kwa madai kwamba kila mmoja alikuwa anafanya mambo kinyume na utaratibu na kila mmoja sasa anafanya kazi peke yake.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, mapacha hao walikuwa wanasherehekea siku yao ya kuzaliwa, lakini kila mmoja alionesha kusherehekea kivyake japokuwa Paul aliposti picha yao ya utotoni.

Taarifa zilisambaa kwenye mitandao kwamba Peter ndio chanzo cha kuvunjika kwa kundi hilo, lakini ametumia ukurasa wake wa Instagram na kukanusha taarifa hiyo.

“Nashangaa kuonekana kuwa mimi ndio mwenye kosa, hakuna ukweli wowote nadhani kosa langu ni kuweka wazi tofauti zetu, ila mimi si chanzo kama watu wanavyosema kwenye mitandao ya kijamii, lakini nashukuru kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa,” aliandika Peter.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad