AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Madawa hayo yalipatikana yamezikwa kwenye shmba moja la ndizi kaskazini mwa nchi, karibu na njia zinazotumiwa kusafirisha cocaine kwenda Marekani.
Rais Juan Manuel Santos alisema kuwa hicho kiwango kikubwa zaidi kuwai kupatikana katika oparesheni moja ya polisi.
Oparesheni hiyo ilikuwa ni sehemu ya kulikabili genge lenye nguvu la Gulf Clan, ambalo linahusika na ulanguzi wa madawa ya kulevya.
Polisi walisema kuwa madawa hayo yalikuwa ni ya Dairo Úsuga, anayejulikana pia kama Otoniel, kiongozi wa genge la Gulf Clan, moja ya magenge hatari zaidi nchini Colombia.
Vikosi vya usalama vimejaribu kumkamta Otoniel kwa miaka kadhaa.
Polisi walisema kuwa pia waliwakamata watu wanne na kukadiria kuwa madawa hayo yalikuwa ni ya thamani ya dola milioni 360.
Katika kipindi cha miezi mwili iliyopita, vikosi vya usalama vimemakama tani 20 za cocaine huko Antioquia.
Genge la Gulf Clan liliibuka kutoka kwa makundi ya mrengo wa kulia ambayo yalitawanyika mwaka 2006 kufuatia msamaha wa serikali.
Serikali inasema kuwa zaidi ya wanachama 1,500 wamekamatwa mwaka huu na kamanda wake wa cheo cha pili kuuwawa
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK