AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Polisi wametumia mabomu ya machozi kudhibiti mamia ya watu waliokuwa wanataka kuingia kwa nguvu kwenye uwanja wa Kasarani ambako zinafanyika sherehe za kuapishwa Rais Uhuru Kenyatta.
"Haki yetu, Haki Yetu," walipiga kelele watu hao ambao wengi wao walikuwa wamevalia nguo za rangi za chama tawala cha Jubilee walipokuwa wakisukumana kutaka kuwapita polisi.
Maofisa wa polisi waliwazuia watu hao wakawapiga baadhi na kuwaacha wakiwa majeruhi. Baadhi walipata tiba ya huduma ya kwanza wakati walioumia zaidi walisafirishwa hadi Hospitali ya Taifa ya Kenyatta.
Polisi walionekana wakiwakimbiza baadhi ya watu wakati wengine walipita kwa nguvu kwenye milango.
Kulikuwa na farasi na magari ya kubeba wagonjwa. Ulinzi ni mkali na wahudhuriaji wote lazima wapekuliwe kuingia ndani ya uwanja huo ambamo wageni kutoka nchi 20 – wakuu wa nchi au mawaziri – wamehudhuria.
Hata hivyo, kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga, aliyesusia uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26 amesusia sherehe hizo na badala yake alikuwa amepanga kuhutubia mkusanyiko mwingine mkubwa eneo la Jacaranda kwa ajili ya kuwakumbuka wafuasi wao waliouawa wakati wa maandamano hivi karibuni.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK