Rais Mugabe Ametaka Kurudishwa kwa Hukumu wa Kifo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais Mugabe Ametaka Kurudishwa kwa Hukumu wa Kifo
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, ametaka kurudishwa kwa hukumu ya kifo nchini mwake kwani watu wanacheza na maisha ya watu kwa kuua wenzao.

Rais Mugabe ametoa taarifa hiyo alipokuwa kwenye mazishi ya mwanasiasa mwenzake mjini Harare, na kusema kuwa sheria ya kunyongwa irudishwe kwani watu wanacheza na kifo kwa kuua wenzao.
“Acha turudishe hukumu ya kifo, watu wanacheza na kifo kwa kuua wenzao, hivi hii ndio sababu ya kuikomboa nchi? Tunataka nchi hii iwe ya amani na furaha, sio nchi ambayo watu wanauana”, amenukuliwa Rais Mugabe.

Taarifa zimeendelea kueleza kwamba kauli hiyo imekuja kufuatia taarifa ya Waziri wa Sheria kusema kuwa zaidi ya watu 50 wameomba nafasi ya kazi ya kunyonga watu mwezi uliopita.
Tukio la mwisho la kunyongwa mtu hadi kufa nchini humo lilikuwa mwaka 2005 baada ya mtu aliyekuwa akifanya kazi ya kunyonga kustaafu, ambapo mpaka sasa zaidi ya wafungwa 90 wapo wanasubiri hukumu ya kifo.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad