Simba, Yanga Kutumia Uwanja wa Azam Complex

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Simba, Yanga Kutumia Uwanja wa Azam Complex
Mechi za wikiendi hii za Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara zinazozihusu Simba na Yanga zitachezwa Uwanja wa Azam FC Complex, Chamazi mjini Dar es Salaam.

Hiyo inafuatia uwanja wa Uhuru kuwa na matumizi mengine ya kijamii na wakati huo huo, Uwanja wa Taifa bado haujaruhusiwa kwa matumizi kufuatia ukarabati wa eneo la kuchezea.
Yanga watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons ya Mbeya Jumamosi wakati Simba wataikaribisha Lipuli ya Iringa Jumapili katika michezo ya Ligi Kuu raundi ya 11.

Taarifa kutoka bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema kwamba kwa sababu hiyo mechi hizo zimepelekwa Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Baada ya mechi 10 za awali, Simba SC wapo kileleni kwa pointi 22, sawa na Azam FC wanaokaa nafasi ya pili kwa kuzidiwa wastani wa mabao, wakati mabingwa watetezi, Yanga SC wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 20.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad