AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mhe. Magufuli amesema hayo leo wakati akiweka jiwe la Msingi la Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoani Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kuungana na Serikali kuhamia mkoani humo ambako ndio makao makuu ya nchi.
''Natoa onyo kwa watu wote wanaotoa takwimu zisizokuwa sahihi wachukuliwe hatua kali za kisheria ambazo tumezitunga wenyewe na kuzisaini, ili kukomesha matatizo ambayo yanatokea kutokana na kutolewa kwa takwimu zisizo rasmi, yoyote anayehitaji kujua takwimu afike sehemu husika ya chombo hicho,'' amesema.
Kifungu namba 37 cha sheria ya takwimu, kifungu kidogo cha 3 hadi 5 kinaruhusu mtu au taasisi yoyote inayotoa takwimu isiyokuwa sahihi afungwe miezi 6 hadi miaka 3 pamoja na faini ya milioni moja hadi milioni kumi au vyote kwa pamoja.
Magufuli pia amesisitiza ofisi ya Takwimu kuendelea kutoa takwimu sahihi kwa lengo la kuwapa taarifa makini wananchi ambazo zitasaidia kuonesha hatua za maendeleo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK