AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamanda Haule amesema Kijana huyo aliyejulikana kwa jina la Msigala Salum (24) amekatwa masikio yote mawili na wananchi wenye hasira kali baada ya kumlawiti mtoto huyo mwenye umri wa miaka mitatu katika eneo la Majengo Mapya Kata ya Lubaga Manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga.
"Tukio hilo limetokea Disemba 20, 2017 majira ya saa tatu asubuhi ambapo kijana huyo anayejishughulisha na shughuli ya kuosha magari mkazi wa Ndala, alimdanganya mtoto huyo wakati akicheza na wenzake nyumbani kwao, kutokana na tukio hilo mtuhumiwa alishambuliwa na wananchi kabla ya Jeshi la polisi kufika eneo la tukio na kumuokoa", amesema Kamanda Haule.
Aidha kamanda Haule ameongeza kwa kusema kuwa mara baada ya tukio hilo baba mzazi wa mtoto huyo alimkamata mtuhumiwa na kumkata masikio yote mawili kwa kutumia kisu na kukimbia, na jeshi la Polisi bado linaendelea kumtafuta.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Ungekata na pumbu zake
ReplyDelete