AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Agizo hilo la kufanyiwa uchunguzi limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo, ameagiza kufanyika uchunguzi wa haraka kwa mkurugenzi huyo baada ya kutoridhishwa na miradi ya maendeleo aliyoitembelea.
Mussa Mpiri anadaiwa kushindwa kutoa ufafanuzi wa fedha zilizopokelewa na Halmashauri hiyo kiasi cha sh.milioni 1.6 ya mapato ya ndani. Imeelezwa pia zaidi ya asilimia 90 ya matumizi ya pesa hizo hayafahamiki hivyo kutia shaka juu ya utendaji wake.
Kufuatia hatua hiyo Waziri Jafo, ameagiza kitengo cha uchunguzi na ufuatiliaji kilichopo Ofisi ya Rais TAMISEMI kufika haraka ndani ya Halmashauri hiyo kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini mwenendo wa Mkurugenzi huyo.
Jafo amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kufahamu kwamba wao wapo kwa niaba ya wananchi wanyonge hivyo wanapaswa kulinda na kusimamia rasilimali za Halmashauri hiyo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK