AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hope Solo ameweka wazi mpango wake huo wa kuwania nafasi hiyo ya kuongoza soka nchini Marekani huku akieleza moja ya sababu kubwa ni kuporomoka kwa kiwango cha timu za taifa za soka za wanawake na wanaume.
Rais wa USSF wa sasa Sunil Gulati ametangaza kutogombea tena nafasi hiyo akitaja sababu kuwa ni kuwajibika baada ya timu ya wanaume kushindwa kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi. Gulati mwenye umri wa miaka 58 amekuwa rais wa USFF tangu 2006.
"Nilipokuwa msichana mdogo, kitu pekee nilichotaka ni kucheza soka na kuichezea timu yangu ya taifa katika ngazi zote na nimefanikiwa kufanya hivyo, kinachofanya ni kulitendea haki taifa langu na kurejesha heshima ya soka kwa kuwa rais wa USSF”, amesema Hope Solo.
Hope ameongeza kuwa katika muda wote ambao amekuwa mchezaji na hata baada ya kustaafu amekuwa akijifunza kutoka kwa marais wengine duniani hivyo ana uhakika amepata uzoefu wa kutosha kuweza kuisaidia nchi yake.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK