Mkoa wa Njombe Waongoza kwa Maambukizi ya Ukimwi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mkoa wa Njombe Waongoza kwa Maambukizi ya Ukimwi
 Mkoa wa Njombe umetajwa kuongoza kuwa na asilimia 11.4 ya watu wanaishi na virusi vya Ukimwi huku Zanzibar wanaoishi na virusi hivyo ni chini ya asilimia 1.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa ametoa takwimu hizo leo Desemba 1 katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambayo Kitaifa imefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Dk Chuwa amesema mkoa wa Lindi umekuwa wa mwisho kwa watu wenye virusi  vya ukimwi na  idadi ya asilimia  0.1 huku maambukizo kwa Jiji la Dar es Salaam yamepungua hadi kufikia asilimia 4.7 ikiwa na maana watu 133,971 wanaishi na ugonjwa huo.

Mkurugenzi huyo amesema kwa ujumla watu 1.4 milioni nchini Tanzania wanaishi na virusi vya Ukimwi na takwimu hizo ndiyo rasmi hivyo asitokee mtu au kikundi cha watu kupotosha.

"Nasema kwa sababu kuna watu wanakurupuka na kuja na takwimu zao. Naomba watambue takwimu ni fani kama fani nyingine na zina miiko yake," amesema Dk Chuwa

Hata hivyo, Dk Chuwa amesema Serikali haimzuii mtu au kikundi kufanya utafiti ila ni lazima awasiliane na ofisi ya takwimu wapitie dodoso zake kabla ya kuruhusiwa kufanya.

Amesema atakayekiuka na kupotosha takwimu adhabu yake iliyowekwa kisheria ni kifungo cha miaka mitatu au faini Sh10 milioni au vyote kwa pamoja.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Justin Mwinuka ameiomba Serikali kutengeneza Sheria zitakazoratibu upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARV).

Mwinuka amesema uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuwabana watu wanaofanya biashara kupitia dawa hizo.Amesema wagonjwa wengi hawapati dawa kutokana na kushindwa kumudu gharama.

"Tuna changamoto ya uhaba wa dawa na zinazopatikana zinauzwa sasa wagonjwa wanashindwa kupata fedha za kununua,"

Mwinuka pia ameomba watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kuingizwa kwenye mpango wa kaya maskini Tasaf ili waweze kutatua changamoto ya uhakika wa lishe.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad