AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Pia, ameeleza alivyopata upinzani kutoka kwa dada yake ambaye hakutaka aolewe na mwanamume aliyemchagua.
Ndoa ya Shilole ilizua gumzo baada ya kufanyika katika hali ya kushtukiza licha ya kuwa aliahidi angefunga kwa uwazi na kufuatiwa na sherehe kubwa.
Shilole akizungumza na mwandishi wa mtandao wa Millard Ayo, amesema aliamua kufunga ndoa kimyakimya na mpenzi wake Uchebe baada ya kuambiwa ndoa haitangazwi kwa sababu inaweza kukaribisha uadui.
“Niliambiwa si kila mtu anapenda kusikia jambo jema kama hilo, wengine wanaweza kukufanyia husuda usifanikishe kwa hiyo nikaamua kuwasikiliza lakini haimaanishi kuwa sitafanya sherehe,” amesema.
Akizungumzia familia yake kumzuia kufunga ndoa amesema, “Unajua hayo ni mambo ya kifamilia, nina watoto wawili halafu ananichagulia mwanamume wa kuolewa naye?”
Shilole amesema anatarajia kufanya sherehe kati ya Desemba 25 na Desemba 27,2017.
“Sherehe ya kukata na shoka nitaitangaza siku mbili hizi. Itakuwa ya aina yake kwa kuwa watu watakula, kunywa na vingine kubeba. Itakuwa ya kihistoria,” amesema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK