AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mashirika ya habari nchini Yeman yanayodhibitiwa na waasi wa Houthi yamewanukuu maafisa polisi wakitangazakuwa mwisho wa mzozo wa wanamgambo wahaini na kiongozi wao umekwisha.
Chama cha Saleh cha General People’s Congress (GPC) kimethibitisha taarifa cha kifo cha kiongozi wao kupitia kituo cha runinga cha Al Arabiya TV cha nchini Saudi Arabia.
Picha na video zilizosambazwa mtandaoni zimeuonesha mwili wa mwanamume anayesadikika kuwa ni Bw. Saleh ukiwa na kidonda kwenye paji la uso wake.
Hadi kufikia wiki iliyopita, wafuasi wanaomuunga mkono Bw. Saleh walikuwa wanapigana na wapiganaji wa jamii ya Houthi ambao zamani walikuwa wanamuunga mkono Bw. Saleh dhidi ya Rais wa sasa wa Yemen, Abdrabbuh Mansour Hadi.
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa (U.N) Watu zaidi ya 8,670 wameuawa na wengine 49,960 kujeruhiwa tangu majeshi ya muungano unaoongozwa na Saudi Arabia yalipoingilia kati vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2015.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK