Viongozi 10 wa CHADEMA Wakamatwa na Polisi Iringa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Viongozi 10 wa CHADEMA Wakamatwa na Polisi Iringa
Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa viongozi wa CHADEMA na baadhi wanachama wa CHADEMA Iringa Mjini wamekamatwa na polisi wakihusishwa na uchomaji wa nyumba ya kiongozi wa CCM na ubomolewaji wa nyumba.


Msigwa amelaani kitendo cha jeshi la polisi kuwakamata baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA kwa kuhusishwa na vitendo vya kuuungua kwa nyumba na kubomolewa nyumba na kudai kuwa jeshi hilo kwa sasa lilipaswa kuanza Intelijinsia ili kujua kwanini nyumba hiyo imewaka moto na nyingine kubomolewa kuliko kufanya uchunguzi jambo ambalo linaweza kupelekea kuwatia hatiani watu wasiohusika.

"Polisi Iringa acheni mara moja kamata kamata ya Vijana Iringa Mjini kwa tuhuma za kuchomwa nyumba Moto na kubomolewa nyumba. CHADEMA haina visasi vya damu katika 'struggle' ya Demokrasia Nchini. Kuhusisha uharibifu wa aina hii na siasa ni kukosa weledi na maarifa katika uchunguzi" alisema Msigwa

Aidha Mchungaji Msigwa amesema kuwa kuhusu nyumba kuungua moto huwa kuna vyanzo vingi vinavyosababisha jambo ambalo polisi walipaswa kwanza kutulia na kuvipa nafasi vyombo husika kuweza kujua chanzo cha moto huo, badala ya kuanza kulifanya tukio la kisiasa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad