AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa mkoa, Gelasius Byakanwa kufanya ziara katika halmashauri hiyo na kuzibaini shule hizo.
Ziara hiyo ilifanyika siku chache baada ya MCL Digital kuripoti wanafunzi wa Shule ya Msingi Mitambo kusomea chini ya miti ambapo kiliitishwa kikao cha wadau wa elimu na kutoa ahadi mbalimbali ukiwemo uongozi wa kiwanda hicho.
Akikabidhi saruji hiyo kwa halmashauri, Kaimu Katibu Tawala wa wilaya, Francis Mkuti amesema mkuu wa mkoa wa Mtwara aliitisha kikao cha wadau wa elimu na watu kuahidi vitu mbalimbali pamoja na nguvu kazi ili kuwaondolea wanafunzi adha wanayokumbana nayo na kuwawezesha kupata elimu bora.
“Nishukuru uongozi wa kiwanda cha Dangote, lengo la mkuu wa mkoa ni kuboresha miundombinu ili (wanafunzi) wapate elimu bora na kutuwezesha kutoka katika zile nafasi za mwisho na sisi tuweze kusogea juu, niwakumbushe wengine walioahidi na wao kutimiza ahadi ili kufikia azma tuliyokusudia,” alisema.
“Kila kitu tunafanya kwa hatua, naamini tukimaliza suala la madarasa itafuata miundombinu mingine ikiwemo nyumba za walimu.”
Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri, Fundikira Masamalo amesema saruji hiyo itatumika kujenga madarasa 48 ya shule 10 zilizoonekana kuwa na hali mbaya.
Amesema halmashauri imeshaandaa vikundi vya vijana kwa ajili ya kufyatua matofali yatakayosambazwa katika maeneo yaliyoonekana kuwa na uhaba wa madarasa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK