AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kocha wa Azam FC Aristica Cioaba, amesema hataki timu yake ifanye makosa kwenye mchezo wa raundi ya 16 bora ya kombe la shirikisho nchini dhidi ya timu iliyopanda ligi kuu ya KMC.
Mchezo huo ambao unatarajiwa kupigwa jumamosi hii kwenye uwanja wa Azam Complex, Cioaba ameueleza kuwa ni mchezo muhimu kwa timu yake kutokana na timu hiyo kutaka kusonga mbele ya michuano hiyo.
“Hatutaki kufanya makosa na wachezaji wanafahamu michuano hii kuwa ni migumu kama huweki umakini wa kushinda mchezo basi utapata tatizo kwa kuwa ni mchezo mmoja tu na sio kama ligi'', amesema.
Azam FC inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ilitinga katika hatua hii baada ya kuifunga Shupavu ya Morogoro mabao 5-0. Wakati KMC iliichapa Toto Africans ya Mwanza mabao 7-0.
KMC ni timu iliyopo chini ya Manispaa ya Kinondoni ya kuanzia msimu ujao itaanza kucheza ligi kuu baada ya kufanikiwa kupanda kutoka ligi daraja la kwanza.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK