Mahakama Yamfutia Kesi ya Madai Uhuru Kenyatta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama Yamfutia Kesi ya Madai Uhuru Kenyatta
Mahakama Kuu Jumanne iliamua kwamba mashtaka ya uhalifu au madai hayawezi kufunguliwa dhidi ya Rais juu ya utendaji wake wa kazi katika kipindi ambacho alikuwa madarakani.

Kutokana na msingi huo wa kisheria Jaji Chacha Mwita aliliondoa jina la Rais Uhuru Kenyatta kutoka kwenye kesi iliyofunguliwa na mwanaharakati Okiya Omtatah akipinga uamuzi wake wa kuteua makatibu wakuu na makatibu tawala.

Ingawa Jaji Mwita hakutoa sababu za kuliondoa jina la Rais Kenyatta kutoka kwenye kesi, kwa namna fulani ni kama alikubaliana na maoni ya Mwanasheria Mkuu kwamba Rais ana kinga ya kutoshtakiwa.

"Kwa maoni yangu, jina la Rais halipaswi kuwemo katika ombi hili. Nitaeleza sababu katika hukumu ya mwisho," alisema kwa ufupi.

Mwanasheria mkuu kupitia mwanasheria mwandamizi Jennifer Gitiri, aliomba mashtaka hayo yafutwe na kuondolewa kwa jina la Rais Kenyatta katika suala linalojadiliwa kwamba ni kinyume cha katiba kuanzisha mashtaka yoyote dhidi ya Mkuu wa Serikali.

"Tunasisitiza kwamba rais hawezi kushtakiwa kwani anafurahia kinga ya rais," aliongeza.

Gitiri alimwambia Jaji Chacha kuwa hakuna ulazima kwa Rais Kenyatta kuingizwa katika suala hili kwa kuwa AG ana uwezo wa kuiwakilisha serikali ya kitaifa katika madai yoyote.

"Maombi hayatapata pigo lolote ikiwa jina la Rais Kenyatta litaondolewa katika kesi hii," aliongeza.

Bunge kupitia kwa mwanasheria Mbarak Awadh Ahmed alijihusisha na mjibu maombi mwanasheria mkuu kwamba amewasilisha maombi ya kutafuta kupinga mamlaka ya mahakama kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Omtatah.

Kikundi cha vijana, kilichodai kina maslahi katika kesi hiyo kilimwambia Jaji Mwita kuwa chini ya sheria ya kimataifa, rais aliyeko madarakani, wakuu wa serikali na mabalozi wana kinga ya kutoshtakiwa.

Katika kesi hiyo, Omtatah aliwashtaki Rais Kenyatta, Tume ya Utumishi wa Umma, Mwanasheria Mkuu na Spika wa Bunge juu ya uteuzi wa Baraza la Mawaziri.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad