AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msigwa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akimuombea ridhaa mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni Salum Mwalimu ili aweze kupata kura za ndio kwa wananchi hao siku ya kupiga kura ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri Mkuu mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Mhe. Edward Lowassa , huku akisindikizwa na mameya na Wabunge mbalimbali kutoka UKAWA.
"Watawala wanaendesha nchi kwa 'personality' na badala ya sheria na kanuni. Kwa bahati mbaya sana wale ambao wanategemewa kusema, kukemea pamoja na kuonya wamekaa kimya. Lakini baadhi yetu tumeamua iwe mvua, jua, iwe mabomu ya polisi, vituo vya polisi hata gereza tutazungumza hatutoogopa mtu yeyote", amesema Msigwa.
Pamoja na hayo, Msigwa ameendelea kwa kusema "nchi ya Tanzania imefika mahali ambako kiongozi hawezi kusemwa, Mkuu wa Mkoa hata Spika wa Bunge".
Kwa upande mwingine, Msigwa amewaambia wananchi wa Jimbo la Kinondoni kwamba wakimuona Mbunge anajikomba komba serikalini basi watambue mtu huyo hatambui wajibu wake anaopaswa kuutekeleza au kuufanya.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK