Okwi Alishindwa Kupumua Baada ya Kupigwa Ngumi ya Koo- Haji Manara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Okwi Alishindwa Kupumua Baada ya Kupigwa Ngumi ya Koo- Haji Manara
Mshambuliaji Emmanuel Okwi alipigwa kwenye koo baada ya kupigwa ngumi.

Hali hiyo ilisababisha ashindwe kupumua na kulazimisha mwalimu wake Kocha Pierre Lechantre kulazimika kumpumzisha.

Okwi alipigwa ngumi na beki wa Ruvu Shooting ambaye alitolewa kwa kadi nyekundu.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema mchezaji huyo anaendelea vizuri ingawa alishindwa kupumua baada ya tukio hilo.

“Alipata maumivu baada ya kupigwa ngumi, unajua ngumi ya kisukusuku kwenye koromeo si jambo dogo.

“Lakini tunashukuru anaendelea vizuri na tunatarajia tutakuwa naye kambini maandalizi dhidi ya Azam,” alisema.


Okwi alitolewa baada ya kupigwa kwa makusudi na beki huyo na Ruvu Shooting walicheza kindava wakionekana walikuwa wamepania kuwaumiza wachezaji wa Simba kama ambavyo walicheza kindava katika mechi dhidi ya Yanga ambayo walilala kwa bao 1-0 lakini mshambuliaji Yohana Nkomola naye alitolewa baada ya kuumizwa na hadi sasa ni majeruhi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad