Serikali Yafunguka Kuhusu Vipodozi Vilivyosajiliwa Kuingiza Nchini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Yafunguka Kuhusu Vipodozi Vilivyosajiliwa Kuingiza Nchini

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini.



Akizungumza leo bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndungulile amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/217 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango.

“TFDA imekuwa ikichukua hatua zifuatazo kudhibiti uingiaji na utumiaji wa vipodozi. Vipodozi vyote vinatakiwa kusajiliwa kabla ya kibali cha kuingiza nchini kutolewa mpaka sasa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo ndivyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini, TFDA imefungua ofisi 7 za Kanda kwa maana Arusha, Dar es salaam, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Mwanza, Tabora kwa lengo la kuimarisha ukaguzi,” amesema Dkt. Ndungulile.

“Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/017 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.”

Hatua ya ufafanuzi huyo imekuja baada ya Mbunge Mata ally salum Mbunge wa Shauri Moyo aliyeuliza “wananchi wengi hapa nchini hasa wanawake hutumia vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu pamoja na jitihada za serikali kuzuia bidhaa hizo Je serikali ina mpango gani madhubuti ya kuzuia vipodozi hivyo.?
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad