Steve Nyerere "Siyo Siri Hata Mimi Nimewachoka Bongo Movies"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KOMEDIANI wa Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ anaamini kuwa, soko la sinema za Kibongo haliwezi kubadilika kama sura za waigizaji ni zilezile za kila siku ambazo hata yeye amezichoka.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Steve alisema kuwa, kama kila mtu anapotazama sinema anakutana na sura ya Kajala Masanja, Shamsa Ford, Aunt Ezekiel na wengine, watu wanachoka na mwisho wa siku ndipo linatokea anguko la sinema kama lilivyotokea.

Steve alisema kuwa, inatakiwa ufike wakati wale mastaa wakubwa waachie ngazi na kuwapa nafasi wengine ili watu waone ladha tofauti maana sura zao zimechosha mashabiki.

“Ninachokipigania ni kwamba waigizaji wakubwa wabaki na haki miliki zao, lakini sura za mastaa haohao zinachosha maana hata mimi nimezichoka,” alisema Steve.

STORI: IMELDA MTEMA, DAR
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad