AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Zitto kupitia taarifa yake aliyoitoa leo, imeeleza kuwa lengo la ziara ni kuwashukuru wananchi na kushiriki kazi za maendeleo katika Kata hizo.
Leo, nikiwa pamoja Na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa, Mama Annamarrystella Mallack, Katibu wa Kamati hiyo, ndugu Janeth Joel Rithe, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Sera na Utafiti, ndugu Emmanuel Mvula tumeanza ziara ya mikoa 8 kutembelea Kata mbalimbali ambazo wananchi walichagua Madiwani kutoka chama chetu cha ACT Wazalendo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Lengo la ziara ni kuwashukuru wananchi, kushiriki kazi za maendeleo katika kata, kuzungumza na kamati ya maendeleo ya kata, kuzungumza na wananchi wa kata husika, kuangalia utendaji wa madiwani kutokana na matarajio ya wananchi, kuona vikwazo na changamoto za Madiwani wetu, kusisitiza Uwazi, Uwajibikaji na Ushirikishwaji wa wananchi kwenye masuala yote ya Kata, pamoja na kufanya tafiti juu ya masuala ya kisera pamoja na miradi ya maendeleo ambayo ACT Wazalendo Taifa tunaweza kuyabeba kusaidia madiwani wetu.
Ziara itafanyika kwa siku 19 katika mikoa 8 husika, ambako leo tumeanzia Kata ya Kiparang’anda, Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani.
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Kiparang’anda
Mkuranga
Pwani
Februari 19, 2018
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK