Benki Kuu Yapunguza Riba kwa Mabenki ya Biashara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Benki Kuu Yapunguza Riba kwa Mabenki ya Biashara
Benki kuu Tanzania imepunguza kiwango cha riba kwa mabenki ya biashara kufikia asilimia 11.


Hatua hiyo inadaiwa itawezesha mabenki ya biashara kupunguza gharama za kukopa fedha benki kuu hivyo kutoa uwezekano wa kupunguza riba kwa wateja wao pia serikali ilichukua hatua ya kupunguza kiasi cha fedha ambacho mabenki ya biashara ilikuwa ikitunza Benki Kuu(Statutory minimum reserve ratio) kutoka asilimia 10 mpaka nane ili kuziwezesha benki kuwa na fedha zaidi kwa ajili ya kukopesha.

Katika hatua nyingine, riba za dhamana za serikali zimepunguzwa kufikia wastani wa asilimia sita, hatua hiyo itapunguza mabenki kufanya biashara na serikali na badala yake kuwakopesha watu wa kawaida kutokana na faida ya kuikopesha serikali kuwa ndogo sana ukilinganisha na kukopesha watu wa kawaida.

Naibu gavana wa Benki kuu, Dr. Kibesse amesema benki kuu imekuwa ikichukua hatua hizo ili kuwawezesha wananchi wamudu kukopa ndio maana kiwango cha riba kimekuwa kikishuka.

Akiwa kwenye kikao na wafanyabiashara Ikulu Juzi, Rais Magufuli alielezea azma ya serikali kufanya fedha yake kuwa ngumu kwa mabenki ili warudi kwa wananchi ikiwemo kupunguza kutoa hati fungani za serikali kwa mabenki
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad