AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Q chief ametoa kauli hiyo akiwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz inayorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV baada ya kupita siku kadhaa tokea msanii huyo kuzimiwa MIC kwenye 'show' ya kuwakaribisha kwa mara nyingine katika tasnia ya muziki Papii na mzee Nguza kutokana na kupotea kwa miaka mingi kwa machoni mwa mashabiki na wapenda burudani wa dansi.
"Wakati mimi nina 'perfom' wimbo wangu wa kwanza katika 'show' wa nikilala naota, nilipata baraka zote kutoka kwa MC wa shughuli, Papii na Baba pia. So kwenye kazi unapoona watu wanamuitikio mzuri inabidi ujiongeze kutokana na wao kuonesha mapenzi yao hivyo mimi nimefanya kazi yangu kama vile ninavyofanya sehemu nyingine kwasababu nina nguvu nyingi katika kazi zangu lakini baadae wakati napanda juu nikashangaa kati kati ya wimbo nimezimiwa kipasa sauti 'MIC'", amesema Q chief.
Pamoja na hayo, Q chief ameendelea kwa kusema "sitaki kuweka kama kulikuwa na tofauti lakini kama zilikuwepo basi nilikuja kujizua baada ya kuangalia zile video tena na watu wa karibu pamoja na mke wangu kuniuliza ni jambo gani lilikuwa linaendelea mpaka kutokea vile. Lengo langu lilikuwa ni kutoa burudani, kumfariji rafiki ambae alipotea machoni mwangu kwa muda mrefu kwa mapenzi yote lakini MIC ikazimwa, sio kosa la Papii wala Mzee wangu Nguza kwasababu wao hawaitahi 'stress' bali ni kosa la ambaye alikuwa fundi mitambo 'technical' aliyekuwepo nyuma anashughulikia masuala ya vyombo vyote"
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK