Mchungaji KKKT Akamatwa na Polisi, Ahojiwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mchungaji KKKT Akamatwa na Polisi, Ahojiwa

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limekiri kumhoji Mkuu wa pili wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi Kilimanjaro Kati, Mchungaji Fred Njama.

Hatua ya polisi kumkamata na kumhoji Mchungaji Njama inakuja ikiwa zimepita siku chache tangu kiongozi huyo wa kiroho kutaja mambo sita aliyodai yanaitafuna nchi.

Akizungumza na Mwananchi leo Machi 17, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Hamis Issah amesema; “suala hilo limeshughulikiwa na kamati ya ulinzi ya wilaya na mimi bado halijanifikia ili niwe na nafasi nzuri ya kulizungumzia.”

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba amesema; “suala hilo siwezi kulizungumza katika simu.” Huku akimtaka mwandishi kufika ofisini kwake na atalizungumzia.

 Akiwasilisha taarifa yake ya hali ya usharika katika mkutano mkuu wa  21 wa usharika huo wa Kiranga,  alitaja mambo hayo kuwa ni kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari, hali ya uchumi kuwa ngumu, miili ya watu kuokotwa, kuminywa kwa vyama vya siasa na ukosefu wa ajira.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad