Wachezaji wa Yanga Waliokua Kambini ya Taifa Waelekea Morogoro Kuungana na Wenzao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wachezaji wa Yanga Waliokua Kambini ya Taifa Waelekea Morogoro Kuungana na Wenzao
Wachezaji wa Yanga waliokuwa kambini na timu ya taifa, Taifa Stars, leo wanatarajia kusafiri kuelekea mkoani Morogoro kujiunga na kikosi chao kinachojiandaa na mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Singida United.

Yanga imeweka kambi Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Singida United utakaopigwa Aprili Mosi 2018 kwenye Uwanja wa Namfua, mjini Singida.

Ibrahim Ajib, Hassan Kessy, Kelvin Yondan na Gadiel Michael wataondoka mchana wa leo kwenda Morogoro kuungana na wachezaji wenzao ambao wameweka kambi maalum mjini humo.

Golipika Ramadhan Kabwili, hatoweza kusafiri kutokana na majukumu mengine ya kuitumikia timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, inayojiandaa na mchezo wa kufuzu kuelekea AFCON U20.


Ngorongoro inajiandaa kucheza mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON U20 dhidi ya DR Congo Machi 31 2018 utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad