AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Habari za awali zilidai kwamba, Pretty kwa sasa yupo kwenye wakati mgumu kwani amefukuzwa katika nyumba aliyokuwa akiishi kisa mwenye nyumba hataki mpangaji anayevaa nusu utupu.
“Mambo ni magumu sana kwa Pretty kwani amepewa ‘notice’ kwenye nyumba aliyokuwa akiishi maeneo ya Sinza, sasa ndiyo anahaha kutafuta pa kuishi, kiukweli tangu amefungiwa amejikuta akipoteza dira kabisa,” alidai rafiki wa Pretty.
Risasi Jumamosi lilimtafuta Pretty ili kujua ukweli ambapo alipopatikana alifunguka kwa kuthibitisha madai hayo na kueleza kuwa amepewa ‘notice’ ya kuhama kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.
“Ukweli ni kwamba tangu nimefungiwa na naibu waziri nimekuwa nikinyanyasika sana, hapa baba mwenye nyumba kanifukuza na kwenye sehemu niliyokuwa nimelipia kwa ajili ya biashara nako amenifukuza, naumia kwa kweli maana nimeshabadilika lakini bado watu wananiona ni mvaa nusu utupu tu,” alisema Pretty na kukiri kuwa kwa sasa anahaha kutafuta nyumba ya kuishi
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK