Mchungaji Msigwa amchana Kitila Mkumbo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mchungaji Msigwa amchana Kitila Mkumbo
Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kumchana Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof. Kitila Mkumbo na kusema kuwa anashindwa kutafuta namna ya kuwatua wamama ndoo kichwani amekazana kuandika barua za kuwajibu maaskofu.


Msigwa amesema hayo bungeni na kudai kuwa serikali imekuwa ikipandisha watu vyeo na kuwapa nafasi watu wengine ambao hawaendi kuleta tija katika nafasi hizo kutokana na kukosa uzoefu wa kazi au kukosa uelewa wa mambo, jambo ambalo amedai limepelekea halmashauri nyingi kufanya vibaya.

"Kwenye taifa letu kunapofanyika promotion au appointment au replacement kwenye eneo lolote haitegemeani na merits, unapomchagua Katibu Mkuu wa wizara unamchagua kwa vigezo gani unataka akaongeze thamani gani, unapomchagua Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya unawachagua kwa vigezo gani, tulilalamika wakati serikali hii inaingia madarakani kwamba mmewatoa wakurugenzi waliokuwa wazuri waliokuwa wanafanya kazi kwa waledi katika ofisi zao lakini wakaletwa watu tu kwa sababu wanavaa sare za CCM na leo tumeona jinsi ambavyo halmshauri zetu zinavyoshindwa kufanya kazi, kumekuwa na ubaguzi wa hali ya juu sana na upendeleo kwa sababu hawa wote walioteuliwa hawaendani na kazi walizopewa" alisema Msigwa

Mchungaji Msigwa aliendelea kutolea ufafanuzi hilo kwa kumtolea mfano Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo

"Kwa mfano ofisi ya Katibu Mkuu ni ofisi serious kabisa unamuona mtu kama Prof. Kitila Mkumbo badala ya kushughulika na namna ya kumtua mama ndoo kichwani yeye amekazana anaandika kuwajibu maaskofu ambao wanashughulika na roho za watu mtaani, badala ya kukaa kwenye ofisi, haya ndiyo tunayosema mtu hajui anaenda kuongeza thamani gani na nimezungumza mambo ya replacement haya unamchukua mtu kama Kitila anazungumzia mambo ya elimu unampeleka kwenye mambo ya maji anakaa ofisini badala ya kuzungumza mambo ya kumtua mama ndoo kichwani ambalo ni wazo zuri yeye anakazana anaandika anataka kumjibu askofu kwa sababu ya mawazo aliyotoa kwamba hakuna demokrasia nchi hii" alisisitiza Msigwa

SOMA PIA: Job Opportunity at Jane Goodall Institute Tanzania, Program Accountant


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad