AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na EATV, Mch. Msigwa amesema kuwa madai hayo hayana ukweli wowote na kueleza iwapo lisemwalo lipo basi muhusika amtafute katika namba aliyoitoa na ikishindikana amfuate Bungeni.
“Mimi nitamtambuaje huyo mtoto, hiyo picha wameweka tu, ilipoanzia ni kwa Jerry Muro ndio ameanza kusambaza hizo habari kwamba mimi ni mwanamke aliyeenda kwa Makonda amejieleza ndio nimemuacha,” amesema Mch. Msigwa.
“Ninachokijibu pale, nakijibu kitu ambacho ameanzisha Jerry Muro, kwamba kuna mtu nimemtelekeza amekuwa akinitafauta na nimekuwa nikimzuia, nimejibu kwamba kama huyo mtu huyo yupo nimekuwa nikitoa namba zangu za simu na kama sipatikani aje hapa Bungeni,” amesisitiza.
Kuanzia mwanzo mwa wiki hii mamia ya wanawake walijitokeza ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ili kupata msaada wa kisheria baada ya kutelekezwa na wazazi wenzio. Pia RC Makonda ametoa nafasi ya kuwasikiliza wanaume waliotelekezwa na wake zao ambapo watapatiwa msaada wa kisheria.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK